Fashion

Thursday 26 May 2016

KAGAME CUP HALI SI SHWARI CECAFA KUSAKA MUANDAJI MPYA

Na steve sameo

Msemaji wa TFF  Alfred Lucas amesema wamekataa ombi la CECAFA, kwakua wana mambo mengi ya kuyasimamia hivi sasa moja wapo ikiwa ni ushiriki wa klabu ya Yanga kwenye hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF.


“Hatukuwahi kusema kama tutaandaa michuano ya mwaka huu, na ndiyo maana tulipokutana na Katibu Mkuu Nicolas Musonye, nikaweka wazi msimamo wetu mwaka huu tumebanwa sana hivyo tunawaomba CECAFA, kuzungumza na nchi nyingine ili kuandaa mashindano haya,”amesema Lucas.

Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Zanzibar lakini baadaye chama cha soko ZFA, kilikataa kutokana na ukata wa fedha za kuandaa mashindano hayo na CECAFA kuiomba TFF, ili kuokoa kutofanyika kwa mashindano hayo mwaka huu.

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :