Fashion

Sunday 9 October 2016

SIMBA MAANDALIZI YA KAZI ZAIDI YA WAKUSANYA KODI WA MBEYA



Klabu ya Simba inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki mkoani Iringa ikiwa njiani kuelekea Mbeya kwa ajili ya kucheza na Mbeya City kwenye pambano la Ligi ya Vodacom msimu huu.

Katibu mkuu wa Simba Patrick Kahemela amesema wanataka kuanza safari hiyo mapema kwa ajili ya kuwapa mapumziko wachezaji wao na ili waweze kushinda mchezo huo unaotarajiwa kuwa mgumu kutokana na ushindani uliopo.

“Maandalizi yetu yanaendelea vizuri na kwa kasi tuliyoanza nayo tumepanga kwenda mapema Mbeya lakini tunapitia Iringa kwa ajili ya mchezo mmoja wa kirafiki pia kuwasalimia mashabiki wetu ambao hawajaiona timu yao kwa muda mrefu,” amesema Kahemela.

Kocha Omog ametoa tahadhari kwa wachezaji wake kuwa makini katika michezo ya mikoani kwani wanaweza kujikuta wanavuruga rekodi yao ya kutofungwa kutokana na ushindani na ubovu wa viwanja vya mikoani.

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :