Fashion

Saturday 11 February 2017

BARAZA LAPITISHA ZAIDI YA BILIONI 65

. Baraza la madiwini Halmashauri ya wilaya ya Mbeya vujijini mkoani hapa limepitisha Zaidi sh  65 bilioni kwa mwaka wa fedha 2017/18.


Akiwasilisha  bajeti hiyo jana afisa mipango wa halmashauri hiyo Anyambilile Mwandiga alisema bajeti hiyo inalenga kuboresha huduma kwa wananchi ikiwemo huduma za afya,uhaba wa vyumba madarasa,maji na maabara kwa shule za sekondari.

Mwandiga aliongeza kuwa kati ya fedha hizo,ruzuku kutoka serikali kuu ni kwa ajiri ya mishahara ya watumishi, matumizi mengineyo na maendeleo ni sh 62 bilioni Huku mapato ya ndani ikiwa ni sh 2 bilioni.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Abihudi Fungamtama alisema bajeti hiyo imelenga kutekeleza miradi mbalimbali ambayo imetengewa fedha.

“hii bajeti itaenda kupunguza baadhi ya changamoto ambazo wananchi wanakumbana nazo hasa uhaba wa madawa,barabara,maji na elimu”alisema Fungamtama.

Hata hivyo mwenyekiti wa halmashauri ya Mbeya Mwalingo Kisemba alisema katika mwaka wa fedha unao isha juni 30 mwaka huu kumekuwa na changamoto ya ukusanyaji wa mapato kutokana na zao la pareto kukosa soko na kuchelewa kwa mvua kunyesha kwani halmashauri hiyo inategemea mapato yake kutoka kwa wakulima.

Aidha Kisemba aliongeza kuwa mwaka wa fedha ujao wamejipanga kuimarisha uzalishaji wa zao la kahawa na pareto ili kuongeza asilimia kadhaa katika mapato yake.

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :