Fashion

Saturday 29 April 2017

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla amezindua mradi wa maji katika kijiji cha Mkola Kata ya Makongolosi Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya uliogharimu zaidi ya shilingi milioni mia tatu tisini na saba.Akifungua mradi huo Mkuu wa Mkoa amewataka wakuu wa Wilaya zote mkoaani Mbeya kuwaondoa watu wote waliovamia vyanzo vya maji.Hata hivyo Makalla amewataka wananchi wa Mkola kuutunza mradi huo na kuhamisha uwanja wa mpira ili chanzo hicho kisiingiliane na shughuli za kibinadamu. Akisoma taarifa mbele ya Mkuu wa Mkoa mkuu wa Wilaya ya Chunya Rehema Madusa amesema ujenzi wa Mradi huo umeanza mwaka 2009 kwa ushirikiano baina ya wananchi, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya na Serikali Kuu. Naye Mkurugenzi mtendaji Sophia Kumbuli amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na wananchi wa Mkola watatafuta eneo la kuhamishia uwanja wa mpira Halmashauri itatoa tingatinga kwa ajili ya kusawazisha. Mradi huo mpya utanufaisha zaidi ya wananchi elfu na maji yake hapana magari . Kwa upande wao wananchi wameushukuru serikali kwa kukamilisha mradi huo na kuahidi kuutunza ili kuondoa changamoto iliyokuwa inawakabili.

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :