Beki
Patrice Evra ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kulambwa kadi
nyekundu hata kabla ya mechi kuanza katika michuano ya Eurpa League.
Evra
beki wa zamani wa Man United ambaye anakipiga na Marseille alikuwa
akijiandaa na mechi dhidi ya Vitoria de Guimaraes, wakati akipasha
alimrukia teke shabiki.
Shabiki
huyo alimtolea Evra maneno ya shombo na kusababisha ashindwe kujizuia
na kwenda kumrukia teke jambo ambalo lilifanya mwamuzi amtoe kwa kadi
nyekundu hata kabla ya mechi.
Vitoria de Guimaraes walishinda bao 1-0 dhidi ya timu hiyo ya Evra ambaye alikuwa jukwaani.