Mwalimu wa Mbeya City, Nsanzulwimo Ramadhani raia wa Burundi amewataka
wachezaji wake kutowafikiria Simba kama timu kubwa katika mchezo wao wa
kesho ndani ya Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya huku akisema hawatatumia miguu yote 24 kwa wakati mmoja hata kama wao ni wakubwa.
Simba
na Mbeya City zinatarajiwa kukutana kesho katika Uwanja huo huku Simba
ikiwa na kumbukumbu ya msimu uliyopita ikiwalaza kwa bao 2-1.
Nsanzulwimo amewaambia hayo wachezaji wake muda mfupi baada ya mazoezi yao kumalizika katika uwanja huo asubuhi ya leo.
"Kama mpo tayari kushinda katika mchezo wetu wa kesho dhidi ya Simba naomba msifikirie fedha za usajili wao kwani hautacheza na badala yake wanaocheza ni wachezaji kama nyinyi wenye miguu sawa na nyinyi.
"Nitafurahi
sana mkijiamini kwa kutokua na wasiwasi juu yao na mkacheza kama ilivyo
kwa mechi zingine zilizopita tutapata matokeo mazuri," alisema
Nsanzulwimo.
Pia
Nsanzulwimo amesikitishwa na kitendo cha kumkosa kipa wake namba moja,
Owen Chaima kutokana na kupewa taarifa za kufungiwa na Bodi ya Ligi ya
TFF.