MADRID WAENDELEA KUTESEKA NA KIPIGI CHA WATOTO WA POCHETINO
Magoli mawili kutoka kwa
Dele Alli na la tatu kutoka kwa Christian Eriksen yalionyesha tofauti
kwa Spurs huku Real wakiendelea na kiwango dhaifu
Mshambuliaji
wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ameikingia kifua timu yake baada ya
kufungwa 3-1 na Tottenham katika uwanja wa Wembley.
Magoli mawili kutoka kwa Dele Alli na la tatu kutoka kwa Christian
Eriksen yalionyesha tofauti kwa Spurs huku Real wakiendelea na kiwango
dhaifu katka kampeni hizi.
Hata hivyo, Ronaldo amesisitiza kuwa Spurs hawakustahili kushinda,
kwani goli la kwanza la Alli lilipatikana baada ya Kieran Tripper kupiga
krosi akiwa ameshazidi.
Ronaldo, 32, alikiambia Football Espana: "Makosa? Unapokosa
ushindi, watu huanza kuangalia mapungufu, lakini nipo hapa naongea,
nikionyesha sura yangu kwa niaba ya wachezaji wenzangu, na ninaamini
kwamba mambo yatabadilika.
About Unknown
Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.