Fashion

Thursday 8 March 2018

MSUVA AENDELEA KUPETA KLABU BINGWA AFRICA


Winga wa kimataifa kutoka Tanzania anayekipiga Difaâ Hassani El Jadida ya Morocco, jana ameendelea kuwa tegemeo kwa timu yake baada ya kufunga bao pekee dhidi ya AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.


Katika mchezo huo uliokuwa wa raundi ya kwanza, Msuva alifunga bao pekee dakika ya 8 na kuipa nafasi nzuri timu yake  kusonga mbele kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

Bao hilo kwa Msuva linakuwa la nne sasa kuafuatia kufunga mabao matatu 'Hattrick', katika mchezo uliopita dhidi ya Benfica Bissau kutoka Guinea Bissau.

Baada ya matokeo hayo, Difaâ Hassani El Jadida, watapaswa kwenda sare yeyote ama kupata ushindi kwenye mchezo wa marudiano utakaopigwa baada ya siku 10 ama 11 mjini Kinshasa, Congo.

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :