Fashion

Friday 13 January 2017

WAKULIMA MKOANI MBEYA WAMEANZA NUFAIKA NA RUZUKU YA MBOLEA MSIMU WA 2017


Kaya 35,360 za wakulima mkoani mbeya tayari zimeanza kunafaika na pembejeo za ruzuku kwa msimu wa kilimo kwa mwaka 2016/17 ikiwa ni pamoja na mbolea,mbegu bora za mahindi na mpunga.


Akiongea na mwandishi wa gazeti hili katibu tawala msaidizi anaye shughulikia kilimo Chimagu Nyasebwa alisema mkoa umepokea pembejeo za ruzuku tani 3536 za mbolea,tani 265 mbegu za mahindi na tani 150  mbegu za mpunga na kudai kuwa zoezi la ugawaji wa pembejeo hizo unaendelea mpaka msimu wa kupanda utakapo malizika.

“Tani 3536 za mbolea ni pamoja na mbolea ya kupandia na mbolea ya kukuzia na zoezi la ugawaji linaenda vizuri na natarajia baada ya wiki mbili wataalamu wangu waniletee idadi ya wakulima waliyo nufaika na walio kosa ili tujue namna ya kuwasaidia walio kosa, hivyo hivyo serikali mmemlipia mkulima asilimia 30”alisema.

Hata hivyo Nyasebwa aliongeza kuwa utaratibu wa utoaji wa pembejeo ubamedirika ni tofauti na ule ambao wananchi waliozoea hapo awali,kwani mwaka huu serikali imebadirisha mfumo wa utoaji wa vocha za ruzuku kwenda kwenye mfumo wa pembejeo za ruzuku mabapo mwananchi hanunui tena vocha.

Kwa upande wake mkulima wa  kata ya Simambwe Wilaya ya Mbeya vijijini Eston Mwaishungu alilalamikia utaratibu uliyofanywa na serikali wa kubadirisha mfumo wa vocha bila kutoa elimu.

“sisi wananchi uku tupo tumekaa tunasubilia vocha kumbe utaratibu umebadirishwa na viongozi wetu wa vijiji na kata wamekaa kimya na kuto elimisha wakulima sasa tutatambuaje kuwa pembejeo hazitolewi kwa vocha na matokeo yake bei imekuwa kubwa”

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :