Fashion

Sunday 24 December 2017

BARCELONA WAPIGA REAL MADRID KAMA WATOTO

Barcelona wameizidi Real Madrid pointi 14 kileleni mwa msimamo wa La Liga baada ya kushinda 3-0 Clasico ya Jumamosi kwenye uwanja wa Bernabeu 
 
Luis Suarez alianza kufungua ukurasa wa mabao akimalizia pasi ya Sergi Roberto muda mfupi tu baada ya mapumziko, Lionel Messi akiipatia Barcelona goli la pili kwa mkwaju ya penalti baada ya Dani Carvajal kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kuushika mpira uliopigwa na Paulinho.

Real Madrid hawakuweza kujibu mapigo baada ya kupunguzwa watu 10, na Barcelona walimuingiza Aleix Vidal ambaye aliipatia timu bao la tatu baada ya Keylor Navas kushindwa kuujaza mikononi mpira dakika za majeruhi.

Goli la Vidal lilikamilisha siku chungu kwa kikosi cha Zinadine Zidane, ambaye matumaini ya La Liga yanaonekana kuzidi kufifia licha ya kuwa na mchezo mkononi. Barcelona walishangilia ushindi wa tatu mfululizo kwenye uwanja wa Bernabeu kwa mara ya kwanza katika historia.

Kilikuwa kipigo cha kudhalilisha kwa Madrid lakini ni wachache tu walioweza kubashiri ushindi wa mabao 3-0 baada ya kumiliki mchezo kipindi cha kwanza

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :