Fashion

Wednesday 13 December 2017

HAPA MANE PALE MCHEZAJI BORA AFRIKA SALAH EPL NYASI ZAWAKA MOTO


Kiungo mshambuliaji Liverpool Adam Lallana amerejea kwenye mazoezi lakini hatakuwa mmoja wa wachezaji watakaoikabili West Brom. 


Meneja Jurgen Klopp amepanga kufanya mabadiliko tena, hata hivyo, Philippe Coutinho na Roberto Firmino wanatarajiwa  kuanza baada ya kupumzishwa mwishoni mwa wiki.

Hadi sasa Klopp amebadilisha kikosi chake cha kwanza mara 59 kwa msimu huu; ni Manchester United tu mwaka 2002 imewahi fanya mabadiliko mengi  katika historia ya Ligi Kuu .

Kama Westbrom itashindwa kuifunga Liverpool itakuwa imecheza michezo 16 bila kupata ushindi katika mashindano yote, na inakuwa ni historia yao kwa ya muda mrefu zaidi yao.
Albion hawako mbali na eneo la kushuka daraja baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Swansea wiki iliyopita.
Hawajawahi kushinda tangu Agosti na wameruhusu magoli 7 katika dakika 16 za mwisho.

Habari kuhusu hali za Timu

Pamoja na Lallana, Joel Matip (majeruhi wa misuli) na Alberto Moreno (mguu) watahukosa mchezo huo
Craig Dawson anaweza kurejea West Brom baada ya kukosa michezo saba iliyopita. Mchezaji huyo amekuwa nje kutokana na tatizo la goti lakini amerejea kwenye mazoezi na anaweza kuchukua nafasi ya Allan Nyom.


Chris Brunt anaendelea kuimarika kutokana na kuumia nyama za paja akiwa na majukumu ya timu ya Taifa huko Wales lakini Gareth Barry , James Morrison, Nacer Chadli na Matt Phillips watakosekana
Takwimu muhimu

Liverpool haijafungwa katika michezo yao nane ya Ligi Kuu dhidi ya West Brom (W4 D4).
Hata hivyo, baada ya kushinda michezo yao ya kwanza ya Ligi Kuu ya Ligi Kuu dhidi ya Baggies, Liverpool imeshinda tu ya tano 13 (D4 L4) inayofuata.

West Brom wamefunga angalau goli moja katika mechi 6 walizo cheza Anfield (W2 D1 L3), wamefanikiwa kufungua goli nane kwa jumla. 

West Brom imekusanya pointi chache zaidi baada ya michezo 16 ya msimu  huu wa Ligi Kuu tangu msimu wa nwaka 2008-09 (12) kuwahi kufanya vibaya.
The End

Unknown

About Unknown

Author Description here.. Nulla sagittis convallis. Curabitur consequat. Quisque metus enim, venenatis fermentum, mollis in, porta et, nibh. Duis vulputate elit in elit. Mauris dictum libero id justo.

Subscribe to this Blog via Email :