Kamati ya nidhamu ya klabu ya Yanga, italazimika kukaa leo kumjadili mshambuliaji wake Obrey Chirwa.
Chirwa ambaye tayari yuko nchini baada ya kujichimbia kwao Zambia, analazimika kujadiliwa na kamati hiyo ambayo itatoa uamuzi.
Taarifa kutoka ndani ya Yanga zinaeleza, kamati hiyo itatoa uamuzi wa adhabu au la baada ya kujadili.
“Chirwa
hawezi kwenda Zanzibar kwa sasa hadi hapo kamati itakapojadili na kutoa
jibu. Kama hana adhabu atakwenda Zanzibar kama ana adhabu hatakwenda,”
kilieleza chanzo.
Chirwa
aliweka mgomo wa kurejea mapema kwa madai ya kumaliziwa fedha zake za
usajili jambo ambalo hata hivyo, uongozi wa Yanga haukupenda lizungumwe
sana.